Gazeti INJILI Kwenye Internet
http://munishi.com

Tel. 254722602445 E-mail: munishifaustin@yahoo.com
Or fmunishi@hotmail.com

Nairobi Leo

Nairobi Cty


Injili House
Makao makuu ya Gazeti la Injili

Maoni yetu kuhusu mzozo wa Israel na Palestina

Mwanadamu aliyenyimwa haki zake za msingi na akawa hana la kufanya ila kujiua na wale anaowaona kama wakandamizaji, ni makosa kuwahurumia wale aliokufa nao kuliko huyu aliyejitoa mhanga, kwani wote wamekufa.

Muhimu ni kujiuliza kwa nini huyu kijana wa kike miaka 18 ameamua kufanya kitendo hicho cha kuyatoa maisha yake mhanga? Bila kuangalia chanzo, tunaweza kusema au kutenda mambo yatakayochoche wengi kujitoa mhanga na hali ikawa mbaya zaidi.

Vyombo vya habari pamoja na kazi nzuri vinavyofanya huko mashariki ya kati, nasikitika kusema kwamba vinaonyesha kuwahurumia zaidi raia wa Izraeli waliouawa kuliko wanaharakati wanaojitoa mhanga.

Tusijidanganye tatizo la Wapalestina na Wayahudi ni kubwa kuliko linavyotangazwa kwenye vyombo vya habari na hasa vile vinavyowaunga mkono Amerika na sera zao mbovu za kumwita kila mtu Ghaidi.

Waandamanaji wakiwa wamebeba bendera na picha ya kiongozi wa Palestina Yasser Arafat karibu na ubalozi wa Amerika Beirut Lebanon.

Laiti waandishi wangechimba kiini cha tatizo lenyewe na wakemee pale inapostahili, tatizo sasa lingekuwa katika hatua za mwisho kumalizika. Lakini kwa mtaji huu wa vyombo vya habari kujifanya kuwa havifungamani na upande wowote, tatizo ndio kwanza linaanza.

Kwenye suala kama hili ni hatari sana kujifanya uko katikati. Mimi nimeamua kuwa upande wa Wapalestina labda nishawishiwe vinginevyo. Majeshi ya Israeli yakitumia vyombo vya kisasa vya kivita wamezikalia sehemu za Wapalestina wasio na silaha. Mnategemea Wapalestina wafanye nini?

Wamekata tamaa ya kuishi wameamua kujiua, na wanapojitoa mhanga waandishi mnawaona Waisraeli ni bora kuliko Wapalestina waliojitoa mhanga?

Basi waundiwe jeshi lao lenye nguvu sawa na lile la Israeli ili vita ya kweli ianze. Mambo yakiwa hivyo nami nitabadili msimamo wangu niwe katikati bila kufungamana na upande wowote. Lakini kwa hali ilivyo sasa, nawaunga mkono Wapalestina katika juhudi zao za kupambana na wavamizi.

Nairobi Cty

Invesment & Morngage House


Nation Centre
Makao Makuu ya Magazeti ya Nation

Nation hupenda sana kuandika mambo ya siasa na wanasiasa wanasahau jamii yote siyo ya wanasiasa. Mwanamuziki wa injili hajawahi kuwekwa ukurasa wa mbele labda awe ameaga dunia. Na hapo itamsaidia na nini?


Gazeti la STANDARD lasema "Sisi siyo kama NATION Waimbaji wa nyimbo za INJILI ndio wanaoupamba ukurasa wa mbele wa gazeti letu. Jioneeni wenyewe. Lakini kwa upande wa siasa sisi ni KANU DAMU.

KBC

Nalo shirika la utangazaji Kenya KBC wanasema: "Sisi ndio tunaoongoza kwa kuwainua waimbaji wa nyimbo za injili Kenya na Afrika mashariki na kati kwa ujumla."

Maneno yao ni kweli hata kama kuna kasoro za hapa na pale, Ukweli unabaki kwamba wasanii wengi wa nyimbo za injili walisaidiwa na KBC kuwafikia walengwa. Karanja Kimwere akitumia vipindi kama "Sing and Shine" na "Joy Bringer" aliwatumia wasanii kwenye vipindi hivyo na ikawa ndiyo njia ya kusikika nchi nzima na hata nje ya mipaka ya Kenya. Watangazaji wa redio nao walichangia pakubwa katika kuwafanya wasikilizaji wasikize nyimbo za Injili kuliko zile nyingine za kidunia. Ilifikia mahali ambapo nyimbo za Injili ndizo zilizotawala anga la Muziki Kenya na Afrika mashariki, na mpaka sasa bado zinatawala.


Moja ya kanda za video za wasanii mbali mbali wa INJILI waliowahi kuonekana katika vipindi alivyotayarisha Karanja Kimwere mtayarishaji wa vipindi vya kidini KBC.

Wito wetu ni kwa vituo vipya vya redio na Tv: Igeni mfano wa KBC wa kuwainua wasanii wa humu nchini na Afrika kwa ujumla. Inashangaza kuona redio nyingi mpya bado zinacheza nyimbo za wasanii wa nchi za magharibi na kuwaacha wasanii wetu bila chombo cha kuinua sanaa yao. Kuna mtu aliyeanza kuwainua hao mnaopenda kucheza nyimbo zao sasa. La kama hakuanza msingewasikia kama na wasanii wenu wasivyosikika huko katika nchi za magharibi. Wanajiuliza kama vyombo vyao vya habari haviwatambui, sisi tutaanzia wapi hata kugusa sanaa yao?

Na mkifanya fujo mtapambana na hawa ambao hawapokei kitu kidogo. Hawa wote wameokoka. Kwa hiyo ukikutana nao ni mawili uende ndani au wakusamehe baada ya kukusomea maandiko matakatifu ya Mungu. Bwana Asifiwe anayeokoa hata Polisi wa Kenya.


KICC


City Hall Annex


Holly Family Basillica


NSSF Building

Safaricom ndio waliofungua dimba la simu za mikononi Kenya. Bei zao wakati huo zilikuwa kuanzia Kshs. 130,000 ili uweze kuwa na simu pamoja na laini yake. Bei za juu zilifanya huduma hiyo kuwa ya watu wanaojiweza kimaisha hasa wauza madawa ya kulevya pamoja na wanasiasa. Kampuni ya pili ilipoingia kushindana na Safaricom bei zilishuka ghafla kutoka Kshs.130,000 mpaka Kshs. 4,500 tu. Sasa hivi kila mtu anaweza kuwa na simu ya mkononi. Wengi wanaishukuru Kampuni ya KenCell kwa kuiona kama MKOMBOZI, japo Safaricom wanaweka bei zao chini kinafiki ili kuwapa ushindani KenCell ambao hawakuwahi kuuza huduma yao kwa kiwango cha juu kama walivyofanya Safaricom. Wengine husema kwamba hata kama Safaricom watatoa huduma zao bure, hiyo ni kama kurudisha zile nyingi walizochukua hapo awali.

KenCell pamoja na kuwa na mtandao wa kisasa usio na matatizo wakati wa kuunganisha simu, lakini bei zao kwa dakika moja ya mawasiliano ni ghali kulinganisha na kiwango cha mapato ya wengi. Wengi wanalazimika kwenda Safaricom bila kupenda kutokana na malipo rahisi , lakini hatujui ni mpaka lini.KenCell waliangalie hilo kwa makini na hakika wateja wengi watawaunga mkono kwani wao ndio walioleta MAGEUZI ya simu za mikononi Kenya.Wanasema kutangulia siyo kufika. Lakini aliyekutangulia akitumia kutangulia kwake kuchuma kwa wingi, anaweza kukupa ushindani na mapato yake ya awali ambayo sijui kama niyaite haramu au halali. Hapo misaidie kuamua.


Hilton Hotel

Bonyeza hapa kwa picha zaidi NAIROBI LEO 2

sms MessagesGospel tape banned by Dar officials
Nina Ukimwi: Asema KENEDY OCHIENG


KENEDY OCHIENG Bonyeza HAPA kwa picha zaidi 2 3 4

Biblia Inasemaje? Ukimwi Unaua Jiadhari- KENEDY Wewe Unasemaje? Mwinyi Aliibadili Tanzania Wewe Unasemaje? Nation TV Yakosa Mwelekeo Wewe Unasemaje? Siasa na Dini Zitenganishwe? Kweli serikali haina dini? Wewe Unasemaje? Waislam Wampora Mkisto Nyumba Wewe Unasemaje? Nyerere Msingi aloujenga Haufai Tuubomoe? Wewe Unasemaje? Mjue Kaka Paul Wewe Unasemaje? "Nisaidieni Nioe" Asema Jeff WACIAMAWewe Unasemaje? Mkapa Hatoki Muda Ukiisha Wewe Unasemaje? Marandu T.L Ajitoa Kwenye "FORUM"Kisha Akarudi TenaWewe Unasemaje?MUNISHI AZINDUA HERALD Wewe Unasemaje? Majira Wajaribu Kumzima Munishi? Wewe Unasemaje? Professor Oloo Amlaumu Mwinyi Wewe Unasemaje? Taliban Wamefanya Kiungu, Amerika walifanya kishetani Wewe Unasemaje? Philip Ochieng attacks Mkapa- Wewe Unasemaje?Moi Aombewa Amalize Vizuri Wewe Unasemaje?Rodnat Mwenda Amshambulia MunishiWewe Unasemaje? SIKU TATU BAADAYE Majambazi Wamvamia Munishi NyumbaniWewe Unasemaje? NYERERE ALISHINDWA MENGIWewe Unasemaje? Leila Asema Alikuwa ShujaaWewe Unasemaje? Wengi Wampinga Leila Wewe Unasemaje? EAGT Dodoma kunafuka Moshi Wewe Unasemaje? ASKOFU KULOLA AMTIMUA MCHUNGAJI ARUSHA Wewe Unasemaje? Mwazembe Amtetea Kulola NAYE MWAKIPESILE ASEMA EAGT IMEOZA Wewe Unasemaje? Kwa Nini Waislamu Wanalalamika? KITABU HIKI MARUFUKU TANZANIA Wewe Unasemaje? Hofu ya Mabomu Imetanda Dar es Salaam SERIKALI YALAUMIWA KUWANYANYASA WAISLAMU Wewe Unasemaje? Amerika Siyo Mungu WENGI WASEMA IJILAUMU YENYEWE. ISIPOBADILI SERA MAMBO BADO Gazeti la Nation Lasema Kenya Ilikosea Kutangaza Msimamo Haraka. Wewe Unasemaje? NALO GAZETI LA An-Nuur Lamwita Osama Shujaa Na Mpigania Haki Wewe Unasemaje? YESU NI MUNGU? Wewe Unasemaje? Haki za Wanaume Wewe Unasemaje? POLISI TANZANIA WALIUA ZAIDI YA70 HUKO ZANZIBAR Serikali Ilihusika Na Mauaji Ya Raia Wasio Na Hatia Wewe Unasemaje? CCM ILIWAITA WALIOUAWA MAGHAIDI Wewe Unasemaje? Serikali Inayoua Raia Haifai WENGI WANAOMBA MUNGU AIANGUSHE CCM Wewe Unasemaje? Mkapa Asema Nguvu Za Dola Zitamshinda Mungu Wewe Unasemaje? Waziri wa Viwanda TZ Amejiuzulu Wewe Unasemaje? WorldSpace Hawajui Wamlenge Nani Wewe Unasemaje? Dani Hagael Amsaga Askofu Habari Katika Picha Wewe Unasemaje? Mrema Awapongeza Afghanistan Wewe Unasemaje? CUF Kujitoa katika muafaka-Wewe Unasemaje? Gospel tape banned by Dar officials Wewe Unasemaje? Bonyeza kichwa cha habari kusoma Habari, au bonyeza "Wewe Unasemaje?" kutoa maoni yako. Kumbuka! maoni yako yatachapishwa hapo kwa hapo kwenye mtandao, na yatasomwa duniani kote sasa hivi.Tembelea Web Site zetu mpya kwa habari zaidi: http://ktn2.netfirms.com http://nipashe.netfirms.com munishifaustin.netfirms.com http://nation.netfirms.com http://munishi.topcities.com

Faustin Munishi Tell. 25472602445 Nairobi Kenya East Africa
E-mail: fmunishi@hotmail.com  |  munishifaustin@yahoo.com

You are Visitor Number

since 14th February 2001
Check mail at Hotmail
Check Mail at Yahoo