![]() ![]() |
||
|
Wamasai wanaohubiri kwenye Redio Biblia Husema maarufu kama Shonara Ole Riambati na Samiet Ole Leteipan wameigiza kipindi "Hakuna nuru gizani" Bonyeza hapa chini usikize kipindi. MASAI:
Hakuna Nuru Gizani!! Lakini hii haiwapi haki serikali ya sasa kulibomoa kanisa la MAXMAM MIRACLE CENTRE. Pamoja na kwamba Muiru amekiri kutokuwa na hati ya kumiliki eneo lilipojengwa kanisa, kama walipata kihalali hakuna mwenye haki ya kuwanyanganya kwa kisingizio cha barabara. Picha inaonyesha wazi kwamba barabara ziko mbili na kuna nafasi kubwa katikati na pembeni kuiongeza barabara husika bila kuharibu mali za raia na hasa makanisa ambayo ni mahali pa kumwabudu Mungu. Dunia na Vyote ni mali ya Mungu. Inashangaza kuona kwamba ili wahubiri wapatiwe sehemu za kujenga makanisa, lazima wajipendekeze kwa wanasiasa. Tatizo ni wakati wanasiasa wanapotolewa madarakani na wengine kuingia. Dunia ya Mungu chini ya sheria za wanasiasa. Mpaka lini tutaendelea kunyanyaswa kwenye dunia ya muumba wetu? Hivi kweli sehemu za kuabudia zinaweza adimika kiasi ni lazima tuwapigie magoti wanasiasa? Wao waliumba dunia gani mpaka kibali cha kujenga mahali pa kuabudia watoe wao? Hatupingani nao, ila wafanye waonavyo ni vyema. Lakini wajue Mungu mwenye dunia na kila kitu mpaka maisha yao anawatizama. Hawawezi kutudanganya kwamba tuna UHURU wa KUABUDU wakati kupata sehemu ya kuabudia ni kitendawili. Sheria hutungwa na watu kwa ajili ya watu. Sheria zinapotumika kuwabomolea watu mali zao, ni wakati wa watu kutunga sheria nyingine za kuwajengea watu mali zao. Amri za Mungu hazibadiliki kwani hazina makosa. Sheria za wanadamu zinatakiwa zibadilishwe kila mara kwani wanadamu wana makosa mengi. Nini kinachowafanya mfikiri kwamba sheria za sasa hazina makosa?
KWAMBA TAFSIRI YA SHERIA INAWEZA PINDISHWA ILI IWAADHIBU WANAOTAKIWA
KUADHIBIWA NAYO HILO NDILO LINALOTUPA MASHAKA. JE! NIA YA SERIKALI
NI KWELI KULINDA SHERIA NA UTENGAMANO AU KUWATAFUTA WALIOIUNGA MKONO
SERIKALI YA AWALI ILI WAADHIBIWE. SERIKALI YA SASA INATAKA KUUNGWA
MKONO. JE INATAKA WANAOWAUNGA MKONO SASA NAO WAJE WAADHIBIWE NA SERIKALI
IJAYO? AU WATATAWALA MILELE? KILA LA KHERI.
Tuma picha na maelezo kwa munishi@munishi.com ![]() http://munishi.com FREE! Send photo and information to munishi@munishi.com
Redio
Injili FM Hii ni redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Yesu ni nuru ya ulimwengu, Alikuja tutoke gizani. Giza na nuru hazikai pamoja. Yaani hakuna nuru gizani. Mungu anakupenda jinsi ulivyo. Ukimwamini na kutubu makosa yako utaokoka. Huwezi kuokoka ndipo uamini baadae. Hapana. Kwanza unaamini, kisha unatubu, na ndipo Mungu anakusamehe na kukupa uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu. Uwezo wa Mungu ndani yako ndio wokovu. Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Ukisha pokea msamaha wa dhambi, omba lolote kwa Mungu na maombi yako yatajibiwa. Katikati yako na Mungu ni Yesu peke yake. Siyo Mchungaji wala Askofu. Omba mwenyewe kwa jina la Yesu, na Mungu atakujibu maombi yako. Baraka za Mungu hazinunuliwi kwa pesa. Huwezi kumhonga Mungu ndipo akubariki. Mungu ni tegemeo letu sote. Wachungaji na washirika, tunatakiwa kumtegemea Mungu kwa baraka zetu. Siyo wachungaji wawategemee washirika kwa baraka zao, huku wakiwaambia washirika wamtegemee Mungu. Nani walio katika nafasi nzuri zaidi kumtegemea Mungu? Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Je baraka za Mungu
zinawezaje kumpita mchungaji ziwaendee washirika ili washirika wambariki
mchungaji? Siku hizi washirika wanawinda baraka zao kutoka kwa wachungaji,
Wanasahau kwamba hata wachungaji wanawinda baraka zao kutoka kwa washirika.
Wanajiunga na makanisa yaliyovuma ambayo wachungaji wake wanatembelea
magari makubwa na kuishi kwenye mitaa ya kifahari. Lengo ni ili na
wao wafanikiwe kimaisha. Wakifika wanashangaa kukuta mchungaji anawategemea
ili wayalipie maisha yake ya kifahari. Walienda kutafuta mafanikio,
wanarudi wakiwa masikini kuliko walivyokuwa. Walikosea lengo. Tunatakiwa
kumtafuta Mungu kwanza, na hayo mengine tutazidishiwa. Hiyo ndiyo
INJILI. Jiunge na kanisa kwa lengo la kuutafuta uhusiano wako na Mungu.
Usijali kama kanisa hilo lina watu wengi au la. Nani alikudanganya
kwamba wengi hawawezi kuwa wamepotea njia? Jiunge na wale wanaomtafuta
Mungu kwa moyo wao wote hata kama ni wachache. Sikiliza
sauti yake UPONYAJI Unaisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Hujambo msikilizaji. Tunamshukuru Mungu kwa ulinzi wake maishani mwetu. Ndiyo maana tunamtukuza na kumwabudu siku zote. Shetani ni muongo. Lazima tupambane naye kila iitwapo leo. Anatumia kila mbinu kuwapotosha watu wa Mungu, Lakini Bwana Yesu asifiwe kwani tumezigundua hila zake. Alifikiri akiwatumia wale wanaojiita wahubiri hatutamgundua. Alijidanganya. Tunajua kwamba yeye huweza kujigeuza na kuwa kama malaika wa nuru. Hatujali atatumia nani, lakini tukiziona dalili zake popote na kwa yeyote tutamkemea arudi kuzimu. Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Kifo cha Yesu msalabani na hatimaye kufufuka siku ya tatu kilimaanisha mengi kwetu tunaomwamini. Sasa tunapokea msamaha wa dhambi, Wokovu wa roho, Uponyaji wa mwili, na baraka maishani Bure. Mtu asikufanyie sarakasi, mbembwe, vitimbi, eti akusukume uanguke ndipo upokee uponyaji. Injili ya Yesu inasimamisha haiangushi. Shetani kazi yake ni kuangusha kwani mwenyewe alianguka kitambo. Ukiona mahali watu wanaombewa na kuanguka anguka hovyo ujue shetani ana mkono wake hapo. Kama nguvu za Mungu ndizo zinazowaangusha, mbona mhubiri huwa haanguki? Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Wengine wanasema wanafanya miujiza kumpita Yesu. Sawa. Je kiutakatifu pia wamempita Yesu? Nina mashaka kama hata wanamkaribia.Hii ni mbinu ya shetani kuongeza chumvi kwenye injili. Tunaikemea katika jina la Yesu ishindwe. Ndiyo ninaamini kwamba Yesu anaponya. Tatizo langu ni watu wanaotumia uponyaji wa Mungu kujinufaisha kibinafsi. Mungu ndiye anayeponya na siyo mhubiri. Uponyaji wako unategeme Mungu na wewe kuliko mhubiri. Hata kama ana nguvu za kuangusha watu, na pengine siyo nguvu za Mungu, haina maana kwamba wewe utapona kwa kuitumia imani yake. Haiwezekani. Kama hujaisikia injili vya kutosha imani yako ijengeke, hata ukiangushwa mara ngapi. Haitaleta tofauti yeyote. Utaangushwa uanguke, ukiamka utakuwa umepoteza pochi na viatu, lakini bado utakuwa mgojwa kuliko mwanzo. Ukimuuliza huyo mhubiri wa vituko, mbona hujapona, utaambiwa kwamba hujatoa fungu la kumi. Utauza gari na shamba ulete pesa zote kwa mhubiri huyo tapeli, lakini bado hali yako itazidi kuwa mbaya. Ni mpaka uijue kweli ya Injili ndipo utawekwa huru. Kweli inasema kwamba kwa kupigwa kwa Yesu wewe ni mzima. Siyo kwa kuangushwa chini. Pole sana. Unaendelea kuisikiliza redio Injili FM, inayokutangazia katika masafa ya INTERNET www.munishi.com Yesu katika mahubiri
yake hakufanya maonyesho tunayoyaona na wahubiri leo. Alihubiri na
kufundisha kweli ya Mungu, walioamini walimwendea ili awaponye, aliwaambia
wapokee kadiri ya imani zao.Yesu hakuwahi kuwaombea wagonjwa wakakosa
kupokea uponyaji wao. Tena Yesu hakutumia imani yake kuwaponya wagonjwa.
Kila mara aliwauliza waliomwendea kama wanaamini anaweza kuwatendea
wanayohitaji. Walipojibu ndiyo, aliwaambia wapokee kadiri ya imani
zao. Leo hii wahubiri wanawaita wagonjwa waje wawaombee siyo wawahubiriwe
injili. Ndiyo maana wengi hawaponi. Huwezi kupona kwa kuitegemea imani
ya mhubiri.Unatakiwa uwe na imani yako. Imani kwako itakuja baada
ya kusikia Neno la Mungu. Unataka mafundisho ya injili uijue kweli
ikuweke huru. Wacha kuwa na imani tegemezi kwa wahubiri. Imani zetu
zinatakiwa kumtegemea Mungu pekee. Ukiiamini Injili, Utubu usamehewe,
halafu Mungu akupe uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu, Huwezi kuangushwa
kwa madai kwamba unaombewa. Utamuomba Mungu kwa imani yako, na Mungu
atakuponya. Soma neno la Mungu kila siku, kwani ndilo litakalokujenga
kiimani. Imani yako ikikua, utawaona wengine wakiangushwa na kudanganywa
lakini wewe utasimama imara. Yesu alipomfufua Lazaro ilibidi atumie
imani yake kwani Lazaro hakuwa hai kuamini. Wewe uko hai. Imani yako
inahitajika sana katika kusababisha muujiza wako. Sikiliza
sauti yake Wimbo
mpya CCM imewatesa wengi MASAI:
Hakuna Nuru Gizani!! Washirika
Nairobi wa nani? Kundi linalowafadhili wahubiri si watu wengi. Wakiamua kuhama itakuwa vigumu kwa wahubiri kumudu gharama za juu kuendeshea huduma zao.Inasemekana kwamba wahubiri wanaoonekana kwenye TV gharama zao ni Kshs.500,000 kwa juma moja. Sasa matajiri wazito wakihama kama walivyomhama Muiru, Sishangai kumsikia akisema kwenye TV kwamba Bwana amemwonyesha kwamba yule mtu ambaye kanisa limejengwa kwenye shamba lake, asarende hati za kumiliki shamba hilo kwake mara moja, kwani hiyo ni amri kutoka juu kwa Mungu mwenyewe. Wengi walishitushwa na kauli hiyo na wakabaki wakijiuliza nini kitafuatia baada ya kusarenda hati za kumiliki mashamba? Pengine kitakachofuata ni kusarenda wake zetu kwa wahubiri. Mungu asaidie tusifike hapo, lakini kila dalili zinaonyesha tunaelekea hapo. Maisha ya hali ya juu yamewalewesha wahubiri na hawataki kushuka. Lakini Mungu atawashusha. Wengine wamefikia hatua ya kujitengenezea kile watakachokiita miujiza kwenye TV. Wanachaguliwa watu watakaosema kwamba wamepona ili kuvuta umati kanisani. Wakija wasipone, wanaondoka kimya kimya. Kwa sababu TV bado inatumika kuwatapeli, kila siku hawakosi watu wapya. Wanakamuliwa, wakikauka wataondoka wapishe wengine. Yaani mtindo wa makanisa umegeuzwa na kuwa kama gari la abiria. Linabeba likishusha na hakuna abiria wanaoweza kusema gari ni lao. Makanisa nayo hivyo hivyo yamekuwa ni mali ya wachungaji na familia zao. Washirika hawana lao. Wanachopata ni mafundisho yenye chumvi nyingi, ikiwashinda kumeza, wanaambiwa wameze kwa lazima ya Mungu. Wanatoa na hawaruhusiwi kuuliza pesa hizo zinatumika vipi. Yani Kanisa ni kama KIOSK ya Mchungaji. Anafungua KIOSK asubuhi saa kumi na mbili. Wanaingia kwa maombi ya asubuhi, maarufu kama "Morning Glory" Sadaka asubuhi lazima watoe. Mchana wanakuja maombi ya mchana maarufu kama "Lunch Time Meeting" Hapo pia wataahidiwa ahadi za baraka kutoka kwa Mungu, lakini wao wanapaswa kumbariki Mchungaji wao anunue BENZ ya milioni kumi na tano. Jioni bado watakuja kuombewa baraka pamoja na kupakwa mafuta, kisha wataulizwa kutoa ili kiwanja cha kanisa kinunuliwe. Bei ya kiwanja wataambiwa ni milioni 30 pesa za Kenya. Kila mtu atatoa mpaka akose nauli ya matatu kurudi wanakoishi. Usijali kama kweli kuna kiwanja kinachonunuliwa, au pesa hizo zinatumika kujenga nyumba ya kibinafsi ya mchungaji katika mtaa wa Karen, na hata kama kiwanja kikinunuliwa, na tuna mashaka kama kitanunuliwa, kitakuwa kimesajiliwa kwa jina la mchungaji na siyo Kanisa. Hata washirika wakiamua kumtimua Mchungaji, Hawawezi kulipa madeni ya mamilioni ya shilingi kanisa linayodaiwa na vyombo vya habari ambavyo hurusha vipindi vya mchungaji huyo. Watajiuliza mbona tunachangishwa kila siku kulipia vipindi? Kumbe kwa makusudi Mchungaji halipii vipindi hivyo ili kuwazuia washirika wasije wakawaza kumtimua wachukue usukani Kanisani hapo. Kwa Mchungaji mkimtimua atachukua mkoba wake aondoke awaachie kiwanja ambacho siyo mali yenu, Tena hakuna dalili zozote kuonyesha kwamba kiwanja husika kinatarajiwa kuwa mali ya kanisa, Nadhani wengi watazimia kuambiwa kwamba kiwanja hicho hakijalipiwa chochote. NI ugumu huo ndio unaowafanya washirika wakose nguvu ya kudai haki zao. Nasi tunauliza. Mpaka lini wahubiri matapeli wataruhusiwa kuwaibia watu mchana machoni pa Serikali na kila mtu?
Bonyeza
hapa usome zaidi
Waruinge
Atawazwa Uchungaji Komba
Ajikomba na CCM
Gospel Television Moto wa kuotea mbali
Ikiwa ndio kwanza inajitayarisha kurusha matangazo yake, GTV imekuwa tishio kwa Serikali Tanzania. Aliyekuwa Rais wa kimabavu nchini humo William Benjamin Mkapa aliamuru polisi wawatie mbaroni wote watakaopatikana na VCD za GTV. Kisa ni kwamba Gospel Television ilikuwa imezungumzia uwezekano wa Mkapa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kutumia madaraka vibaya. GTV ilikuwa imedai kwamba, Mkapa akiwa madarakani aliwaamuru POLISI wawaue Wazanzibari zaidi ya 70 kwa kosa la kusema CCM Chama Cha Majambazi hawakitaki. Pamoja na mambo mengine GTV ilipendekeza tume ya kumchunguza Mkapa iundwe na akipatikana na makosa sheria ichukue mkondo wake. Pia GTV ilidai kwamba Mkapa aliitawala Tanzania kama mali yake binafsi kwani hakutaka ushauri wa mtu yeyote. Bado msimamo wa GTV ni huo na hatuombi msamaha kwa Mkapa wala CCM. Habari Zaidi Hotuba ya Munishi kwa TAIFA ![]() ![]() ![]() ![]() ![]() ![]()
|
||||||||||||||||||||||||||||||
|
|