Apollo
Joo Afariki
Ni
baada ya kuugua kwa muda mfupi



Marehemu Apollo Joo
Tumezipokea
kwa majonzi na masikitiko makubwa habari za kifo cha mmoja kati
ya waanzilishi wa makanisa ya kipentekoste Kenya, mchungaji Justus
Odera Oyombe, maarufu kwa jina la apollo Joo
Atakumbukwa zaidi kwa mahubiri yake ya kusisitiza msimamo katika
ukristo.Majuma machache kabla ya kufa kwake Apollo alisema.Eee
Yesu mwana wa Mungu uliye hai. Nimefanya kazi yako tangu ujana
wangu, na kama binadamu nilikukosea mengi.
Neema yako imekuwa ikinifunika na kunihakikishia kuwa bado hujaniacha
pamoja na udhaifu wangu kama Apollo.Ikikupendeza nije kwako, basi
ya nini mateso haya mwilini?
Kazi uliyonipa nimeifanya kwa kadiri ya uwezo wangu kama binadamu.Makosa
yote niliyokukosea Naomba unisamehe na na uwasaidie wote niliowakosea
neema ya kutosha kunisamehe kama na mimi ninavyowasamehe wote
walionikosea.
Nijalie usingizi mwema nkingoja siku ile utakayomwamsha kila aliyelala
katika wewe ili auingie ufalme wako wa milele.



Atakumbukwa
daima kwa Imani yake kwa Mungu kupitia mwanawe Yesu Kristo.