Ukurasa wa mbele
Gazeti la injili
Nyimbo za Munishi
Soma barua Yahoo
Soma barua Hotmail
Tuma SMS duniani
Sema nami
Sikiliza waongo
Twende kanisani
Gazeti INJILI http://munishi.netfirms.com
E-mail: munishifaustin@yahoo.com
Or fmunishi@hotmail.com

Mkapa Hatoki Muda Ukiisha 2

Ukurutu Apendekeza

Mi mawazo yangu ni kuwa Mzee Small au King Majuto au Jangala mojawapo angefaa sana kuwa rais. Kwani ukizingatia hali halisi ya ukapa iliyopo Tanzania hivi sasa tunahitaji Rais atakayerejesha Kicheko majumbani. Mi naenda zangu ----- Lets Be Honest -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 10 | Joined Nov. 2001 | Posted on: 8:42 pm on Nov. 19, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Ima Amuunga Ukurutu Mkono

Mheshimiwa ukurutu, hapo umenena! Na hasa haswa akiwa mzee small. Nadhani tutasahau ukapa wote!. -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 5 | Joined Nov. 2001 | Posted on: 10:54 pm on Nov. 19, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Mchunguzi Awachunguza Wote

Kama kawaida yake akiona mambo yanaenda asivyotaka huingilia kati.

ukurutuu samahani mh .... nadhani walioanzisha bodi hii walikuwa na lengo tofauti kidogo na wewe. ndio maana kukawa na mgawanyiko wa hoja mbali mbali ..siasa na mengineo . sasa mheshimiwa utanisamehe nikitumia usemi wa mvunja nchi ni mwana nchi na hii inajithihirisha pale ninapozichambua kauli zako. mh ukurutuu lazima tukubali wakati mwengine kutoa point za changamoto ni muhimu na sio kila kitu ni utani tuu. naweza kusema sio kila lazima mtu uzungumze tuu hata kama huna cha kuzungumza ..wakati mwengine nakubaliana na wahenga waliosema kuzungumza ni kipaji . mh lazima tuwe serious .kama ujisikii kuandika kaa kimya haitakupunguzia kitu . asalaam ----- BY MCHUNGUZI -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 33 | Joined Oct. 2001 | Posted on: 12:01 pm on Nov. 20, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Ukurutu Achachamaa

Unaonyesha ulivyo na utumwa wa Mawazo. Hivi unaifahamu katiba ya nchi kweli wewe Mchukuzi? Kumradhi Mchunguzi. Kwanini Umeona Kuwa ni Kioja kwa Mzee Small au King Majuto kuwa rais. Kwani wale sio watanzania wenye akili timamu? Nimefanya makusudi kwani nimesoma porojo za kuwataja watu hawa na wale kisa alikuwa Waziri zamani au ni Mbunge, Mmesahau kuwa Tanania in maelfu ya watu wanaweza kuwa rais. Sijui Tanzania itabadilika lini. Mimi namsifu Mmoja hapo juu aliyesema tusitaje majina bali tukuze Democrasia. Mwisho naomba uniombe mimi na niliowataja radhi, kwani kusema mimi ni mvunja nchi ni kunidhalilisha mimi na wale niliowataja. Au umeona wana kasoro gani ukilinganisha na uliowataja wewe? Au kuna mtu maridhawa kakutuma umpigie vingoma nini?. (Edited by ukurutuu at 7:48 pm on Nov. 20, 2001) (Edited by ukurutuu at 7:55 pm on Nov. 20, 2001) ----- Lets Be Honest -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 10 | Joined Nov. 2001 | Posted on: 7:59 am on Nov. 21, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Munishi Aangusha Bomu
Asema Nyerere alishindwa

Kiafrika Mtu akishakufa siyo vizuri kuusema ubaya wake maana mwenyewe hayuko kujitetea. Lakini anapokuwa hai, hata kama ni uhai unaosaidiwa na mitambo, bado watesi wanaruhusiwa kuusema ubaya wake ili akipona ajirekebishe.Na asipopona basi itawabidi watesi wanyamaze kimya wawasikilize mashabiki wake wakisema uzuri wa Mwalimu wa kuwakomboa Watanzania kutoka katika minyororo ya ukoloni wa Waingereza na kuwaigiza kwenye ukoloni mwingine wa Julius Kambarage Nyerere.

Ukoloni wa kwanza haukuwa mbaya kuliko huu wa pili,ila tofauti yake ni kwamba ukoloni wa pili uliongozwa na Mwafrika kutoka Butiama, na ule wa kwanza uliongozwa na mzungu kutoka Uingereza. Kwa hiyo tofauti ilikuwa ni viongozi wa ukoloni, na Watanzania hawakutoka katika minyororo ya ukoloni, bali walibadilika kutoka ukoloni huu kungia mwingine ambao ndio unaowatawala mpaka leo.

Kwa watu wenye mawazo kama mimi, ni heri tungebaki kama tulivyokuwa maana msaada wa kweli ungetoka popote, kuliko kujidanganya kuwa tulikuwa salama na kumbe ukweli wa mambo ni kwamba tulikuwa pabaya kuliko mwanzo

.Ilikuwa kama kukimbia mvua na kuingia kwenye kibanda cha nyasi kinachovuja. huwezi kueleza tofauti maana bado unanyeshewa. Na mpaka leo Watanzani kama mimi hatujui tofauti ya kuwa huru na kutawaliwa.

Ikiwa kuwa huru ni kumruhusu Nyerere kujaribia mawazo yake ya siasa ya ujamaa kwenye maisha yetu na baada a miaka 30 atuambie mawazo yake yalishindwa kwa sababu alikosea, na adhabu tuliyompa ni cheo cha baba wa Taifa, basi mtanisamehe nikisema kuwa mwacheni huyo mzee apumzike kwa amani kutoka katika dunia hii, ili akapate nafasi ya kukutana na Muumba wake ambaye akiamua kumsamehe amsamehe.

Na pia akiamua kumhukumu yote ni sawa, lakini siwezi kumwomba Mungu amponye Nyerere aje kufanya nini? Ambacho hakukifanya kwa miaka yote 77 aliyoishi duniani? alitumia nusu ya maisha yake kufanya majaribio na Watanzania,na sasa Mungu atatushangaa kwamba tunamsumbua amponye. Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu, na hawezi kukubali kushiriki utukufu wake na Nyerere.Amewaona Watanzania wanamwabudu Nyerere kuliko yeye na ameamua kumchukua ili wajue kuwa wanaweza pasipo Nyerere.

Tena Yeye Mungu pekee ndiye Baba wa vyote. lakini wanadamu wanamwita mwanadamu baba wa taifa? hiyo ni kufuru. Elimu ni nzuri, lakini ile inayotoka kwa Mungu.Hii ya wanadamu mara nyingi inakuwa na kasoro nyingi.na wale waliyo nayo husahau kumtegemea Mungu,na kuitegemea elimu yao ambayo mara nyingi inashindwa kuwatatulia matatizo.

Elimu ya madarasani na uongozi ni vitu viwili tofauti lakini wanadamu huvutiwa sana na viongozi waliosoma wanasahau kuwa uongozi unatoka kwa Mungu. Na mara nyingi hawa viongozi waliosoma hawaongozi vizuri.

Tuna mifano mingi, lakini Nyerere ni mmoja wa hao viongozi wasomi ambao hawakuongoza vizuri.


Hotuba nzuri, maneno ya kushawishi akili na kupendwa na waandishi wa habari siyo cheti cha kiongozi mzuri. Na Nyerere anasifiwa kwa hiyo.

Lakini ukija kwenye matendo ya zile hotuba nzuri hakuna hata kijiji kimoja cha maonyesho kuonyesha kuna msomi mmoja aliyewahi kufikiri kuhusu vijiji vya ujamaa na hiki ni kimoja ya vijiji alivyovianzisha, na watu katika kijiji hiki wanafurahia mawazo ya msomi huyo.

Lakini Tanzania nzima hakuna hata kijiji kimoja cha ujamaa kilichobaki kama maonyesho ya mawazo ya msomi Nyerere badala yake Tanzania ni moja kati ya nchi masikini duniani. Na yote hayo ni matunda ya msomi mmoja waliyemwita Mwalimu wa umasikini.

Sasa mambo yakiwa hivyo najiuliza kwa nini alipoteza muda kwenda Makerere kupata shahada ya DR. ambayo haikumsaidia kuifanya Tanzania mahali pazuri pa kuishi?

Bado nasita katika njia mbili, sijui nimpeleke mtoto wangu Makerere apate shahada kama ya Nyerere ndipo aje agombee uongozi wa Tanzaia, au tumtegemee Mungu atupe kiongozi ambaye ataongoza vizuri hata kama hana karatasi ya chuo kikuu?

Na kama Mungu anaweza kutupa kiongozi basi hata mimi niko tayari maana kile ambacho sina ni karatasi ya chuo kikuu tu.na kama Nyerere DR. anaweza kushindwa mambo mengi hivyo, basi nina hakika siwezi kushindwa kama yeye.


Kwa Watanzania ni vizuri Nyerere aondoke ili tuwe na mawazo mapya na mbinu mpya za kuikomboa kikweli Tanzania.Hata Musa alipokufa ,Yoshua alifanya makuu kuliko Musa Na Yoshua wa Tanzania ni mimi Faustin S. Munishi
Wewe Unasemaje?

Hayeshi afurukuta

Nimekusikia mheshimiwa Munisi lakini bado kuna mambo sikubaliani na wewe kuhusu mzee Nyerere.Kila binadamu anaouwezo wa kufanya makosa ,sio mzee Nyerere peke yake.Kuhusu matatizo yanayoikabibli Tanzania kwa wakati huu ,hapo umeweza kufafanua kiundani na kiukweli pasi na kufanya upendeleo wa aina yeyote.Lakini swali je wewe kama rais utawezaje kutatua haya matatizo yaliyopo nchini?. ----- www.lycos.com(/D) -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 64 | Joined Oct. 2001 | Posted on: 12:58 am on Nov. 22, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Marandu Akosa Subira

Mimi nashauri hoja ya Ndugu Munishi iondolewe kwani imechukua nafasi kubwa sana katika ukumbi huu lakini density yake ni ndongo mno. labda angesamaraizi na kisha akaondoa hutwo twumatangazo twake. vinginevyo imekaa kama Hekaya za Abunuwasi Simulizi za Esopo au Alfa Lela Ulela. Ni hoja au niite hotuba pengine mahubiri. Na hii sii sehemu ya mambo hayo. -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 65 | Joined Oct. 2001 | Posted on: 6:03 am on Nov. 22, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Eriksen Amkwepa Munishi

Kuna mheshimiwa mmoja au wawili wanaelekea kuwa na mawazo ya kujenga demokrasia; na siyo kumtaja mtu binafsi kugombea uraisi. Hakuna ubaya wowote kumtaja mtu. Tunataka mtu ambaye atapanua na kuimarisha demokrasia; na hasa kutuletea maendeleo. Halafu hayo maelezo ya Munishi inakuwaje? Hapa sio mahali pa mahubiri. Hayavutii kusoma. Kwa maana hiyo hayatawafikia walengwa wote. ----- Eriksen -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 29 | Joined Oct. 2001 | Posted on: 6:13 am on Nov. 22, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Pope Ampuuza Munishi

Kwa kweli huyu Mheshimiwa sana huyu (siwezi kumuita Muinjilisti) Anatubadili muelekeo kabisaaaa hajui anataka kusema nini wala anacho kiongea tutawakilisha maoni kutayarisha Board kwa ajili ya mahubiri. Naomba turudi kwenye Mada Hii ni mada Serious kuliko wanavyo fikiria watu kama Munishi Good Day -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 50 | Joined Oct. 2001 | Posted on: 8:30 pm on Nov. 22, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Mtu Kwao Awatoa Tongotongo

Nani awe Rais Tanzania ni swali ambalo kwa mtazamo wa haraka linaonekana ni rahisi kujibu na ndio maana wengi wameanza kurembea majina kama vile kwipikwipi la kupopolea embe; chochote kinachoanguka ni sawa tu. Kwanza inabidi kuelewa Rais tunamzungumza ni wa Jamhuri ya Muungano na si wa Tanganyika wala Zanzibar.

Pili ni kuhakikisha kuwa Rais huyo ana uwezo na akili timamu itakoweza kumuwezesha kuleta maendeleo na kuwaondoshea dhiki wananchi na sio kuwaongezea mzigo wa maisha na kuwa ombaomba mitaani.

Hivyo tunahitaji kuangalia mtizamo wake wa kisiasa wa mtu huyo. Histora inaonyesha kuwa chaguo la mwalimu Nyerere huwa karaha na kero kwa watanzania.

Maendeleo yanayoonekana sasa ni mtirirko wa uongozi bora wa Mzee Ali Hassan , kama vile kuporomoka kwa elimi Tanzania tunaouona sasa ni sera mbovu za elimu za Nyerere.

Inachukua muda kujua na kuonja matunda ya maendeleo. Lakini baya zaidi nikufanya Tanzania kutawaliwa kwenye misingi ya Kifalme(Kisultani mambo leo). Mfano Baba alikuwa Rais na mtoto nae na shemeji na mjomba. Hatuendi. Mambo ya akina Warioba msiyalete.

Lakini kubwa zaidi tusijifanye kusahau kuwa hii ni jamhuri ya muungano na hivyo wazanzibari nao wanahaki ya kuwa rais wa Tanzania na kwa kweli historia inajionyesha wazanzibari ni wazuri sana katika uongozi na hasa wa kisiasa.

Nahata haya tunayojivunia sasa bara ni matunda yalioletwa na siasa safi za rais Mzanzibari. Mengi yamechafuliwa baada ya kuondoka. Huu ukumbi tunojitapa sasa kufanya mijadala ni matunda ya Mzanzibari,Mzee Ruhsa.

hatutaki kupelekwa tena kule tulikotoka na kuanza kupekuana mifukono kusachi kama unayo Colgate umeficha! Sasa ni zamu ya Zanzibar,iwe imo kwenye katiba au la! mangapi hayamo kabisa kwenye katiba ya jamhuri ya muungano na yamepindwapindwa kunufaisha upande mmoja wa muungano na yamefanyika.

Nitakupeni mfano mdogo na ambao si nyeti sana. Ushirikiano waKimataifa si suala la muungano. Hivyo Zanzibar kwa kutambua hivyo waliweza kushirikiana na mataifa ya nje nakuweza kuptamisaada mingi ya kuendesha nchi yao.

Bara kuona hivyo Zanzibar inanufaika ,wakaigeuza Wizara ya mambo ya nje kuwa Wizara ya mambo ya nje na ushirikiani wa Kimataifa na hivyo kuipiga FULL STOP Zanzibar katika harakati za kujinasua kiuchumi. Missada sasa ikija inaishia bara. Hitimisho RAIS ATAKEKUJA ATOKE ZANZIBAR ----- Kiroboto -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 22 | Joined Nov. 2001 | Posted on: 10:39 pm on Nov. 22, 2001 | IP
Wewe Unasemaje?

Mchunguzi Akurupuka
HAPA AJIDHIHIRISHA ZAIDI

Mtukwao kweli inabidi tumshukuru mzee mwinyi katika kuleta maendeleo kwa upande mmoja . Lakini mkuu napenda kukupinga vikali kabisa kuwa mzee nyerere ndio chimbuko la kuporomoka kwa elimu katika Tanzania .

Mheshimiwa mtukwao, naomba ufanye uchunguzi wa kutosha . Mwalimu Nyerere atakumbukwa na kila Mtanzania katika swala la elimu .

jamani mwalimu amefanya makubwa katika nchi hii sio mtu wa kumzungumza zungumza tuu. kuhusu mzee ruska ... mheshimiwa naona kicheko kama umemwona mzee ruska na serikali yake walikuwa ni viongozi bora.kwa dondoo zifuatazo naomba uniambie kama mbado upo mbado umesimama katika fikra zako.

1. mheshimiwa mtu kwako, katika serikali ya mzee ruska kulikuwa kumekithiri rushwa na uonevu uliokithiri serikali ilikuwa imeenda likizo kabisa.mfano mdogo tuu ni hawa watu wa tume ya jiji walivyokuwa wakituchanganya katika kutugawia watu watano watano kiwanja kimoja . kulikuwa hakuna utu bali fedha.

2. mheshimiwa mtu kwako ,serikali ya mzee ruska ilikuwa iliendeshwa kiswahili mno.serikali ilikuwa aina fedha kabisa . Bajeti ya serikali ilikuwa ikipagwa kwa miezi mitatu mitatu .. hivi serikali gani duniani inafuata utaratibu huu..

3.mheshimiwa mtu kwako,serikali ya mzee ruska ilimsahau kabisa mtu wa kawaida watu kama kina Dewji ,Raza na Gulamali walikuwa majina ya kuogopwa na walikuwa na uwezo wa kufanya lolote.

4. mheshimiwa mtu kwao, serikali wakati wa mwinyi ilikuwa imeenda likizo ,kulikuwa na magulio tuu na kila mtu alikuwa na wazo moja tuu la kuchukua chake mapema...

5.Mheshiwa mtu kwao, serikali ya mzee ruska ilitutesa sana katika kutulipa mishahara yetu , bila kuwasahau waalimu waliumia mno mheshimiwa mbado upo?

6. mkapa amerudisha kitu kilikuwa kimepotea kitu kinachoitwa SERIKALI ...... Mheshimiwa mtukwao ,naomba kutoa hoja kuwa wakati umefika wa kumfikiria kiongozi atakayeweza kuendesha serikali katika karne ya ishirini na moja, nikiwa na maana kiongozi mwenye vision, mkapa kazi yake ilikuwa kurudisha heshima ya kitu SERIKALI nadhani ndio maana anabana sana wananchi. WAKATI UMEFIKA WA kumjenga mtu atayeongoza Tanzania katika msingi ya maendelo ,usawa ,haki na uhuru wa kweli sambamba na matarajio ya kila mwananchi .

MUNGU IBARIKI TANZANIA ............ (Edited by MCHUNGUZI at 11:22 am on Nov. 22, 2001) ----- BY MCHUNGUZI -------------------------------------------------------------------------------- Total Posts: 33 | Joined Oct. 2001 | Posted on: 11:33 pm on Nov. 22, 2001 | IP
Wewe Unasemaje? Endelea Sehemu ya Tatu

 

 
| http://munishi.netfirms.com |
 
<<Back  |  Home |  Gazeti La Injili | Injili2 | Nyimbo Za Munishi | Next >>